England: Hifadhi
kutokana na ubakaji
Karibu nusu ya wanawake
wanaoomba hifadhi nchini Uingereza,ambapo wengi wao wanatoka katika maeneo
ya vita au ya madikteta
wakatili ni waathiriwa wa ubakaji.Hata hivyo,wakati mwingi serikali
haitambui ubakaji na vurugu nyinginezo za ngono kuwa ni sababu za kuomba
hifadhi.Kuanzia wakati wanapowasili,waathiriwa wa ubakaji kwa kawaida
wanakabiliwa na ubaguzi na
chuki za wageni, vyote hivi vikizidisha ubaguzi jinsia ambao waathiriwa
wote wa ubakaji wanaufahamu. Ofisi ya mambo ya Ndani
ya Uingereza inajibu madai ya wanawake kwa chuki na kutoamini, na
kuyakataa madai hayo kuwa ya ‘bandia’.Badala ya kupata msaada na
kuungwa mkono,wanawake na familia zao wanafanywa kuwa masikini kifedha
kutokana na mfumo wa kutumia vocha ambao unawanyima marupurupu.Wananyimwa
pia ushauri huru wa kisheria,kupata huduma za matibabu na huduma
nyinginezo,na kutengwa na uwezekano wa kupata msaada wa jamii.Wanawake
wengi huwekwa hata kizuizini.Fikiria malalamiko ambayo yangeweza kutolewa
kama wanawake wa kiingereza ambao wangelipiga ripoti polisi kuwa wamebakwa
wamefungwa jela! Tunafanya kampeni ya kuleta mabadiliko katika sheria na jinsi zinavyotekelezwa ili kwamba wanawake ambao wanabakwa katika nchi nyinginezo na wanaomba hifadhi hapa wanapata ulinzi wanaotakiwa kupata.Lalamiko la kundi la wanawake wa Global Women of Colour Network wa WinWages wanadai kuwa: · Ubakaji ni lazima utambuliwe kuwa ni usumbufu na mateso,na kwa hiyo
basi ni sababu ya kuomba hifadhi. · Haki ya kupata ulinzi haraka na haki ya kubakia katika nchi hii kwa
wanawake wanaokimbia ndoa
zenye vurugu. · Kukomesha kutiwa kizuizini kwa wanawake walionusurika kubakwa
wanaoomba hifadhi. · Rejesha
marupurupu ya kijamii na marupurupu mengineyo kwa wale walionusurika
kubakwa wanaoomba hifadhi na familia zao.
|
| MGOMO WA WANAWAKE WA DUNIA |