MAONI KUTOKA KIJIJI CHA Kaabong, Uganda

 

Mimi ni mama wa mashambani na kiongozi wa akina mama katika kijiji chetu.  Tangu tujiunge na mgomo, nimeona mabadiliko mengi maishani mwangu.  Mme wangu amenipatia shamba na ana shukulu kazi ninazofanya nyumbani.

Mme wangu alinichukua kama mali yake.  Lakini baada ya mgomo, ameheshimu haki zangu.  Alinipatia ng’ombe mmoja na mbuzi  wawili.  Sasa nina mifugo sita amboyo naweza uza ama nifanye chochote bila kumuomba ruhusa.

 

Mgomo ni silaha kubwa.  Jamii yangu waweza sasa kupata matibabu ya bure.

 

Nina furaha kwamba wanawake na wasichana kutoka zaidi ya nchi sitini wameungana pamoja kupigania haki ya kumaliza kazi nyingi wanazo zifanya,  huduma ya afya, maji masafi na kutotaka vita.

 

Mimi ni mke wa shujaa na nina amini mgomo.  Watoto wangu wawili wakiume waliaga dunia kutokana na vita via ukabila.  Wanawake wengi walichukuliwa kwa nguvu.

 

Mimi ni mama ambaye hajaolewa na nina fanya kazi na huduma ya afya katika kijiji chetu.  Tangu tuwe na mgomo, wanaume katika jamii yetu, waweona umuhimu wa akina mama wenye watoto bila bwana.

 

Mimi ni kiongozi katika mtaa wa Lolelia na ninaunga mkono nia za akina mama za kutaka dunia iwe mahali patulivu pakuishi.  Nawaomba wanaume wote duniani waunge mkono mgomo wa akina mama.

MGOMO WA WANAWAKE WA DUNIA

Ukurasa wa nyumbani (Home)